²Ù±ÆÊÓƵapp

Redirecting...

²Ù±ÆÊÓƵapp

The Africa Renewal website has relocated to:

You are being redirected automatically. If not, click the link above.

Jamii zinazostawi zinahitaji mshikamano wa kijamii, haki na ujumuishwaji

Get monthly
e-newsletter

Jamii zinazostawi zinahitaji mshikamano wa kijamii, haki na ujumuishwaji

Barani Afrika, Huduma za Misaada za Kikatoliki zinasaidia jamii ‘kushughulikia kile kinachozigawanya ili ziweze kupata kile kinachoziunganisha’ na kwa pamoja kufanyia kazi mabadiliko ya kimageuzi.
Zipporah Musau
Afrika Upya: 
5 January 2024
Zara Ellie, mama na mjasiriamali aliyejitolea, akiongoza mkutano wa Jumuiya ya Akiba na Ukopeshaji wa Ndani ya 'Hanoune' huko Koudoul, Chad, ambapo wanachama huungana ili kukuza ukuaji wa kifedha na mshikamano.

Bi. Nell Bolton ni mkurugenzi wa kiufundi wa kitengo cha Usawa, ujumuishwaji na Ukuzaji Amani katika makao makuu ya Huduma za Misaada ya Kikatoliki huko Baltimore, Marekani. Katika Sehemu ya II ya mahojiano yake na Zipporah Musau wa Afrika Upya, anaeleza ni kwa nini usawa na ujumuishwaji ni muhimu kwa jamii zenye mshikamano: Hapa kuna madondoo kutoka kwa mahojiano hayo:

Ms. Nell Bolton

Ni kwa nini usawa, ujumuishwaji na ukuzaji amani ni muhimu katika jamii leo?

Jamii zinazostawi huanza na mshikamano wa kijamii, haki, ujumuishwaji, na ushiriki.

Ili maendeleo endelevu yatokee, watu wanapaswa kuwa na uwezo wa kusikilizana, kuaminiana vya kutosha ili kuungana na kufanya kazi pamoja na kushirikiana kufikia malengo yao ya pamoja, na ili sauti na ushiriki wa kila mtu uhesabiwe katika mchakato huo. Hivi ndivyo tunavyoifanya kazi yetu.

Tumeweka kipaumbele cha kusaidia watu na jamii kuweza kushughulikia kile kinachozigawanya ili ziweze kupata kile kinachoziunganisha, na kwa pamoja, kufanya kazi kuelekea mabadiliko ya kimageuzi.

Tuliona hili kuwa muhimu kwa sababu tunajua kwamba changamoto kubwa zinazoukabili ulimwengu wetu leo - umaskini, magonjwa, mabadiliko ya tabianchi - hazitatuliwi kwa ubinafsi. Hazitatatuliwa na makundi yanayopingana, au kwa kulipa kundi moja kipaumbele na kulitenga jingine. Matatizo yanapaswa kushughulikiwa kwa pamoja.

Tunaweka kipaumbele ujumuishwaji wa mshikamano wa kijamii na mtazamo wa haki katika programu zetu zote.

Uendeshaji wa misaada ya kibinadamu na maendeleo, pamoja na programu za kukuza amani kwa njia shirikishi ni njia inayopata matokeo ya kimageuzi katika sekta zote. Ni kufanya kazi, na kuona faida, za kufanya kazi katika maendeleo ya kibinadamu na uhusiano wa amani.

Je, usawa, ujumuishwaji, na mshikamano una umuhimu upi katika jamii yoyote ile?

Tunayaona masuala haya kama msingi wa uwezo wa watu na jamii kustawi, na kuandama malengo yao ya maendeleo ya pamoja. Tunaangalia masuala ya usawa na ujumuishwaji kwa utaratibu katika kazi yetu katika suala la ushiriki katika kufanya maamuzi, ugawaji wa rasilimali na matumizi ya rasilimali. Na kujaribu kufanya hivyo kimakusudi.

Ni nini hufanya kazi yako barani Afrika kuwa ya kipekee?

Mojawapo ya nguvu ambazo Huduma za Msaada za Kikatoliki inazo ni upeo na ufikiaji wa uwepo wetu, pamoja na maisha marefu ya programu zetu. Kwa mfano, tumesherehekea miaka 65 nchini Ghana. Hii ina maana kwamba tuna ushirikiano wa muda mrefu na mashirika ya ndani, baadhi yana washirika wa Kanisa Katoliki, baadhi hayana.

Wote wanajulikana sana, wanaheshimiwa sana na wanaaminiwa na jamii wanamoishi na kuhudumu. Mahusiano haya yamejikita katika maono ya pamoja na kujitolea kwa pamoja kwa muda mrefu kwa kanuni za pamoja kama vile heshima ya watu wote, mshikamano, manufaa ya wote, na kuwahudumia walio hatarini zaidi bila kujali dini, rangi au utaifa.

Kwa ushirikiano huu, tumeweza kuimarisha uongozi wa mitaa na kama wakala tunapiga hatua zaidi na hilo katika miaka ya hivi karibuni kujitolea na kuweka kipaumbele kuwa na washirika wetu wa ndani na sauti zao na vipaumbele vyao kuwa mbele. Hili ni jambo ambalo si geni kwa CRS, si la umaarrufu wa kimpito, linatokana na kujitolea kwa kudumu na kwa muda mrefu. Na linaonekana katika ubunifu na ushirikiano mpya wa kusisimua ili kuchochea mabadiliko kwa kiwango kikubwa.

Faida nyingine tuliyo nayo ni kama shirika lenye mamlaka mengi, tunaweza kuelekeza kwa urahisi zaidi migogoro inapotokea kati ya maendeleo ya kibinadamu na kazi ya amani. Na tunaweza kupanga mipango yetu, tunaweza kuunganisha programu zetu, kwa kweli katika wigo mzima, kulingana na vipaumbele na mahitaji yaliyopo, katika kipindi fulani cha muda katika nchi.

Washiriki kutoka jumuiya ya Kiislamu na Kikristo wakishiriki katika Warsha ya Uponyaji wa Kiwewe kama sehemu ya mradi wa Ushirikiano wa Kujenga Amani wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CIPP) unaoungwa mkono na USAID na washirika katika Boda, Jamhuri ya Afrika

Je, programu hizi zinayaathiri vipi maisha ya watu barani Afrika?

Tunaona mara kwa mara katika miradi yetu kwamba tunapoongeza kwa makusudi mshikamano wa kijamii na kuzingatia haki, kuna mabadiliko ya kimageuzi: wakati watu wanaweza kufanya kazi pamoja vyema, basi programu zetu hushuhudia matokeo yenye nguvu zaidi. Ingawa tuna ushahidi wa hafifu wa hili, tumekuwa tukiwekeza katika ajenda ya kujifunza ili kujenga ushahidi mkali zaidi kuhusu mbinu hii.

Tuna tafiti kadhaa za majaribio zinazoendelea kuangalia hii ina athari gani kwa, kwa mfano, lishe shirikishi Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo? Je, ina athari gani kwenye programu za kulisha shuleni nchini Mali? Je, ina athari gani kwa mapato na mazao ya vikundi vya wazalishaji nchini Madagaska?  

Huku uchunguzi huu ukiendelea kuja, kwa sasa tumekuwa tukifanya tafiti za muda mfupi, na ninaweza kueleza baadhi ya yale ambayo tumethibitisha kufikia sasa.

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)

Mnamo 2022 tulifanya mradi wa maendeleo ya vijana mashariki mwa DRC, tukizingatia kipengele cha kuimarisha uchumi wa mradi kupitia jumuiya za akiba na mikopo ya ndani, tunaziita SILC Groups. [Jumuiya za Uwekaji Akiba na Ukopeshaji wa Ndani [Savings and Internal Lending CommunitiesÌý(SILCs) ni aina ya vikundi vya uwekaji akiba vya kijamii ambavyo vinaendeleza utaratibu usio rasmi wa ufadhili mdogo].

Tumejua kwa muda mrefu sasa kwamba akiba katika vikundi ina athari chanya kwa umoja wa kikundi, kitendo cha kuaminiana kiasi cha kukusanya akiba zenu ili kutoa mikopo kwa wanakikundi kwa manufa ya kuinua hali yako ya kiuchumi kwa pamoja kama kikundi kina athari kubwa sana ya uhusiano kwa wanakikundi hao.

Kwa uingiliaji kati huu wa SILC tulianzisha kikundi cha matibabu na udhibiti kama utafiti wa majaribio. Kwa zaidi ya nusu ya vikundi tuliongeza warsha za kuimarisha mshikamano wa kijamii, na mafunzo ya ujuzi wa kudhibiti migogoro pekee. Haya yalikuwa matibabu, na kisha vikundi vingine vya udhibiti vilifanya tu uingiliaji wa SILC. Tuligundua kuwa vikundi vyote viwili bado vilikuwa na athari hizo chanya za uhusiano katika suala la uaminifu wa kikundi, lakini uwezo wa kikundi wa kudhibiti mizozo ulikuwa na nguvu zaidi, chanya zaidi kwa wale waliopata uimarishaji wa mshikamano wa kijamii.

Kilichovutia sana ni kwamba tuliona pia matokeo bora ya kiuchumi kwa vikundi vya matibabu ambavyo vilikuwa na uimarishaji wa mshikamano wa kijamii. Kwa hakika vilishuhudia mafanikio ya takriban 7% katika suala la mitazamo ya ustawi wao wa kiuchumi uboreshaji wa faida ya takriban 7% katika uwekezaji wavyoo katika shughuli za kiuchumi, na kisha matokeo ya kushangaza ya ongezeko la 25% katika shughuli zao za pamoja za maendeleo ya kiuchumi, ilhali kikundi cha matibabu kiliona hali ya kurudi nyuma katika eneo hilo. Tunachokiona zaidi ni kwamba tunapojumuisha uwiano wa kijamii na haki katika mipango yetu ya maendeleo, watu hunufaika kifedha na matokeo bora zaidi ya maendeleo.

Darfur, Sudan

Nitawapa mfano mwingine wa mradi katika eneo la Darfur nchini Sudan. Hii ilikuwa kabla ya mgogoro wa sasa nchini Sudan. Tulikuwa tukifanya kazi na wafugaji na wakulima ambao hapo awali walikuwa kwenye mzozo kuhusu maliasili ya ardhi na maji. Tulikuwa na Mpango mkubwa wa Ustahimilivu, tukifanya kazi na watu wote wawili. Mwishoni mwa Mpango wa Ustahimilivu vikundi vyote viwili vilinufaika kutokana na usimamizi wa migogoro na uimarishaji wa mshikamano wa kijamii mpaka vikundi vyote viwili viliongezeka na kufikia mwaka mzima wa upatikanaji wa ardhi na maji.

Vikundi vyote viwili viliweza kuungana kupitia kamati za usimamizi ambazo zina ujuzi wa kutafakari jinsi vitakavyosimamia rasilimali hizo, kukabiliana na migogoro na kuwa na mahusiano yenye nguvu zaidi, kwa hakika vilishuhudia ongezeko la mwaka mzima la upatikanaji wa ardhi na maji.

Kwa hivyo hizo ndizo aina za athari ambazo huleta mabadiliko katika uwezo wa watu, sio tu kuishi, lakini kustawi.

Sudan Kusini

Sudan Kusini inatoka katika mpango wa Ustahimilivu na Usalama wa Chakula. Katika awamu za awali za kazi hii, timu yetu iligundua kuwa wafanyakazi wenyewe walikuwa wamepitia vurugu nyingi hivi kwamba baadhi ya hatua za uhamasishaji wa kiwewe zingekuwa na manufaa.

Wafanyakazi wa mradi huo walipata mbinu hii yenye nguvu sana katika kuwapa uwezo wa kushughulikia tajriba zao wenyewe za migogoro, vurugu na woga, hivi kwamba walipendekeza kupanua uingiliaji kati kwa washiriki wa mradi. Kwa hivyo, tuliongeza kipengele kwa kutumia ufahamu wa kiwewe na ustahimilivu pamoja na mbinu ya kuimarisha mshikamano wa kijamii CRS inauita B tatu na D nne.

Katika Kiingereza, B tatu zinarejelea: -

  • Kufunga - ni mchakato wa kukuza dharura ya kibinafsi, mageuzi ya kibinafsi, uponyaji wa kiwewe, na kufikia kiwango ambacho sisi kama watu binafsi tuko tayari kushirikiana na wengine. Hili linafanywa kupitia warsha za kustahimili kiwewe, vikao vya kukuza uongozi, na shughuli kama hizo.
  • Kuunganisha - ni mazungumzo ya ndani ya kikundi, kukuza maelewano, kuwaandaa watu waweze kufanya kazi pamoja kwa ushirikiano zaidi, ili waweze kujihusisha na wengine kwa njia yenye kujenga. Hizi zinaweza kuwa fursa za kutafakari historia na utambulisho pamoja na matumaini na maono ya siku za usoni. ï‚·
  • Kuziba- ni mazungumzo na ushirikiano katika vikundi mbalimbali vya utambulisho. Hii inaweza kuhitimishwa na mipango ya vitendo ambayo imepangwa na kuongozwa kwa pamoja, kwa manufaa ya pande zote.

Tunalenga kujenga juu ya uwezo, mali, na uwezo wa watu. Kwa hivyo, warsha hizi zimeundwa ili kuwasaidia watu kugundua kile wanachoweza kuchangia, kile ambacho vikundi vyao vinaweza kuchangia katika manufaa ya wote katika mustakabali bora.

Mawakala wa nyanjani na wanajamii kwa pamoja wameripoti mabadiliko mengi kama matokeo ya mbinu hii rahisi. Watu wana mahusiano ya amani zaidi na wale wanaohusiana nao kwa karibu, na wale wa makabila mengine. Wana ujuzi wa kushughulikia mizozo na ushindani unaozuia maendeleo.

Kwa mfano, kiongozi mmoja wa kikundi cha shamba la vijana aliripoti kwamba chama chake cha watu 50 kutoka koo tofauti kingevunjika ikiwa hawangepata ujuzi wa kutatua masuala yao kupitia mazungumzo. Badala yake, wanaendelea kwa nguvu baada ya miaka miwili. Jamii zimepata njia mpya za kutatua mizozo ya mipaka na migogoro mingine ya ardhi, na kushirikiana katika kujenga barabara mpya na vituo vya maji. Na wana uwezo mkubwa zaidi wa kukabiliana na mshtuko na mafadhaiko, ambayo ni msingi wa ufafanuzi wa ustahimilivu.

Je, ni vipi baadhi ya viambajengo ambavyo vimechangia mafanikio ya mpango wa amani?

Nikikirejelea kipengele kile cha maisha marefu ambacho tulikijadili hapo awali kwamba kuna ushirikiano wa muda mrefu kwa muda. Katika COSOPAX, kwa mfano, mpango huo umekuwa ukiendelea tangu 2013. Huko Mindanao, pia ni suala la kufanya kazi kwa ushirikishwaji na Waislamu, Wakristo, na watu wa kiasili kushughulikia mzozo wa utambulisho.

Pia, si kuacha katika ngazi hiyo ya kimlalo bali kufikiria kimkakati kuhusu jinsi ya kufanya kazi mashinani, katika ngazi ya kati, na katika ngazi za juu ili mabadiliko yoyote, manufaa yoyote chanya yajitokeze katika miundo na katika mifumo. Kipengele cha kuwa na uwezo wa kufikiria kwa viwango vingi kwa wakati mmoja na kuweza kufanya kazi kwa njia kamili ambazo zimechangia athari fulani ambayo tumeona huko.

Afrika ndilo bara changa zaidi huku takriban 70% ya watu wake wakiwa chini ya miaka 40. Ujumbe wako kwa vijana wa Afrika ni upi? ÌýÌý

Kwa vijana wa Afrika, ninyi ndio mawakala wa amani. Ninyi ndio mawakala wa mustakabali wowote ambao mnaweza kuwazia. Na sauti zenu ni muhimu, ushiriki wenu ni muhimu.

Tuna programu katika nchi tofauti kama Ghana, Togo, Misri, Ethiopia, na kwingineko, nje ya Afrika huko Bosnia Herzegovina, Iraqi, na nyingine, tukifanya kazi na vijana kutumia uwezo na nguvu zao, na kuwahamasisha kama Mabalozi wa Amani Vijana.

Tunawapa ujuzi na maarifa katika kusimamia masuala changamano na kukuza amani, pamoja na kuchanganua jamii zao wenyewe na ambapo wanaweza kuleta mabadiliko, tunawaunganisha na vielelezo wa ndani na kisha wanaenda. Wana athari kubwa sana kwa wenzao na kwa mitazamo na tabia za wenzao.

Tumeona mbinu hii ikifaa sana nchini Ghana na Liberia katika kipindi kabla ya uchaguzi, kujaribu kuweka uchaguzi kuwa na nguvu zaidi, na wa amani zaidi.

Tumeona pia nchini Togo, kuweza kuwajibikia baada-mizozo, kufanya kazi pamoja kwa ufanisi katika misingi ya kidini na kupunguza mivutano kati ya vikundi tofauti vya kisiasa na vikundi tofauti vya utambulisho.

Tumeona nchini Ethiopia kutokana na mizozo baina ya jumuiya, katika kuweza kuhamasisha wakazi wenzao kuungana na kujenga baadhi ya barabara zilizoharibiwa na asasi za jumuiya na nyumba zinazohitajika.

Haya yote yanaonyesha athari kubwa ambayo vijana wanaweza kuwa nayo wakati wanaweza kuungana kuyazingiramaono yao chanya kwa manufaa yao wenyewe na ya jamii yao.